Sunday, December 19, 2010

K-Basil saa chache baada ya Kuoa

Mwanamuziki wa Muziki wa Injili Kashumba Basili a.k.a K-Basil akiwa na mkewe bi Perida Mdegella saa chache baada ya Kufunga pingu za Maisha siku ya tarehe 5 Disemba 2010. K-Basil pia ni mchungaji ngazi ya MP Katika kanisa la Glory of Christ Tanzania Church almaarufu kama Nyumba ya Ufufuo na Uzima

Monday, December 6, 2010

K-Basil Aiga rasmi kambi ya makapera!

Mwanamuziki wa muziki wa injili Kashumba Basil (K-Basil) jana ameiga rasmi kambi ya makapera baada ya kuamua kuvunja ukimya na kujitwalia mke.

K-Basil alifunga pingu za maisha siku ya jumapili majira ya saa 9 alasiri katika kanisa la Glory of Christ Tanzania Church maarufu kama Ufufuo na Uzima ambapo ndoa yao ilifungwa chini ya Mchungaji kiongozi wa kanisa hilo Mch. Josephat Gwajima na kuafutiwa na maombi maalumu ya wachungaji kutoka Japani ambao waliibariki ndoa hiyo.

Sherehe ya kukata na shoka ya kuwapongeza maharusi hao ilifanyika kuanzia saa moja usiku katika ukumbi wa Kilimanjaro Park uliopo Sinza jijini Dar es Salaam.

RudishaMusic inawatakia maisha mema na yenye baraka katika ndoa yenu.

Saturday, November 20, 2010

Breaking News: K-Basil mbioni kujitwalia Jiko


Mwimbaji wa muziki wa Injili Kashumba Basili (K-Basil) aliyewahi kutamba katika medani ya muziki wa kizazi kipya (Bongo flava) kama unayoitwa na vijana wengi wa kileo ambaye ameokoka tangu mwaka 2007 anatarajia kufunga pingu za maisha hivi karibuni.

RudishaMusic ilihabarishwa na mwanamuziki huyu kuwa ndoa yake itafungwa tarehe 5 Disemba 2010. RudishaMusic itakuletea habari moto moto kuhusiana na uimbaji wa muziki wa injili wa K-Basil sambamba na matukio ya ndoa yake hivi karibuni.

Thursday, October 14, 2010

Saraphina Urio



Je unafahamu kuwa Dada huyu unayemuona hapa ni muimbaji mahiri wa Muziki wa injili? Endelea kufuatilia RudishaMusic. Saraphina kama mmoja wa "Viriba vipyaa" chenye "Divai mpyaa" atakuja hivi karibuni na albamu yake mpyaa. Tayari wimbo wake uitwao "Sifa zivume" Umeanza kutamba kwa kupigwa mara kadhaa wa kadha katika kituo cha WAPO RADIO katika kipindi cha "zilizotufikia" hapa jijini Dar es Salaam. Saraphina Urio is Coming Soon only at RudishaMusic.

Unataka Kumjua Barnabas zaidi?



Kama wewe ni mpenzi wa muziki wa injili na ungependa kumjua Barnaba zaidi Bofya hapa

Monday, October 11, 2010

Rachel Marlon: Nipo Mbioni kutoa albamu yangu mpyaaa

RudishaMusic imefanya mahojiano na mwanamuziki Rachel Marlon na kutaka kudodosa nini hasa kinaendelea juu ya mipango yake ya kimuziki na haya ndio aliyoyaelezea. "Nipo mbioni kutoa Albamu yangu mpya itakayokwenda kwa jina la SINA HOFU TENA. Albamu hii itachukua muda wa miezi kama mitatu hivi kuwa mtaani kuanzia sasa. Vilevile nafikiria kurekodi video ya hii albamu yangu."

Haya wapenzi wa muziki wa injili kaeni mkao wa kula na kupata ladha mpyaa kutoka kwa dada yetu Rachel Marlon. Albamu yake inarekodiwa katika studio yake mwenyewe. RudishaMusic itaendelea kukujuza juu ya ujio ya albamu hii pindi itakapotoka.

Friday, October 8, 2010

Christina Shusho


Christina Shusho ni mmoja kati wa waimbaji wachache wa muziki wa injili nchini Tanzania wenye kuimba kwa miondoko ya taratibu na kuuvuta uwepo wa BWANA. Moja kati ya vibao vyake vinavyofanya vizuri zaidi katika miondoko hiyo ni "Neno la Mungu".