Monday, September 20, 2010

Jane Misso azindua albamu yake "Uinuliwe"

Saa chache kabla ya kufanya uzinduzi wa albamu yake, Jane Misso alipiga show kali ya kumtukuza YEHOVA katika viwanja vya Tanganyika packers, ndani ya Nyumba ya Ufufuo na Uzima iliyopo Kawe jijini Dar es salaam.
.
Jane Misso kama anavyoonekana hapa akimwaibisha shetani kwa kumnyima sifa kwa kibao chake maarufu "Umoyo" Huku akiimba kwa furaha na kumpatia sifa YEHOVA.
Jane Misso akipiga show yake huku maelfu ya watu wakiimba pamoja naye. Muimbaji huyu alizindua albamu yake siku ya Jumapili, 19 Agosti 2010 katika ukumbi wa Diamond Jubilee. Albamu yake mpya inakwenda kwa jina la "Uinuliwe".

Picha zote kwa hisani ya Ufufuo na Uzima.

Peace Muluu amsindikiza Jane Misso katika Uzinduzi wa albamu yake

Peace Muluu kutoka Nairobi Kenya, muimbaji wa nyimbo za injili
ambaye alishambulia jukwaa pamoja na Jane Misso. Katika picha Muluu akiimba ndani ya Nyumba ya Ufufuo na Uzima.


Peace Muluu akiimba ndani ya Nyumba ya Ufufuo na Uzima, iliyopo kawe jijini Dar es salaam, katika viwanja vya Tanganyika Packers.

Picha zote kwa hisani ya Ufufuo na Uzima.