Wednesday, September 22, 2010

Ulishawahi kusikia Mchiriku wa Injili? Muulize Barnabas Kassian

Kijana Barnabas Kassian hivi karibuni ameibuka na mtindo mpyaaa katika medani ya muziki wa Injili. Kijana huyu ambaye hupenda kujiita Kondo wa Yesu ambaye ni bingwa wa miondoko ya mchiriku ametokea kupendwa sana wa wapenzi wa muziki wa injili huku yeye akiendelea kumpa BWANA sifa na utukufu.

Jina la konda wa Yesu husema mwenyewe “heri kuwa konda wa Yesu kulikoni kuwa msukule”. Unaijua historia ya maisha yake? Endelea kutembelea RudishaMusic tutakuletea makala maalumu itakayomtambulisha Barnaba mwan wa faraja.
Barnabas Kassian akiwa jukwaani katika moja kati ya show zake kali.
Barnabas Kassian akipiga show live ndani ya Nyumba ya Ufufuo na Uzima, kawe jijini Dar es Salaam


Muunge Mkono Jackson Benty

Jackson Benty mwanamuziki mahiri wa muziki wa Injili hapa nchini Tanzania yupo mbioni kununua vyombo vya kisasa vya muziki. Ili kuimarisha na kuendeleza huduma ya uimbaji ambayo Mungu ameipanda ndani yake RudishaMusic inakuomba umuunge mkono kwa kumchangia kiasi chochote ulichobarikiwa nacho na Mungu atakubariki. Kwa michango yote tafadhali wasiliana na Jackson Benty Mwenyewe Kupitia simu yake 0718 255112 / 0757 426721 au mtumie barua pepe
bentyjackson@ymail.com

Jackson Benty Akiimba!